Kuhusu Idara ya Usimamizi wa Maafa
Ofisi ya Waziri Mkuu — Tanzania Bara
Historia
Historia ya Usimamizi wa Maafa Tanzania
Shughuli za usimamizi wa maafa nchini baada ya uhuru mwaka 1961 zilijikita katika kutoa misaada ya kibinadamu kwa waathirika wa maafa kama vile chakula, dawa, mavazi, makazi ya muda, na vifaa vya malazi. Shughuli hizo zilitekelezwa na serikali kwa kushirikiana na taasisi zisizokuwa za kiserikali zikiwemo Chama cha Msalaba Mwekundu na taasisi za kidini. Vilevile, Serikali ilikuwa ikishirikiana na taasisi za kimataifa zikiwemo Shirika la Chakula la Umoja wa Mataifa na Shirika la Oxfam.
Pamoja na Serikali kushirikiana na taasisi zisizo za kiserikali na taasisi za kimataifa lakini katika kipindi hicho hakukuwa na taasisi ya serikali iliyokuwa na jukumu la moja kwa moja la usimamizi wa maafa. Vilevile, hakukuwa na muundo wa kitaasisi, sera, sheria na miongozo ya uratibu wa maafa. Kutokana na kuongezeka kwa matukio na madhara ya maafa nchini Serikali iliandaa mfumo wa kisera na kisheria ili kuimarisha shughuli za uratibu maafa nchini. Kwa kuzingatia hali hiyo Serikali ilitunga Sheria ya Uratibu wa Utoaji wa Misaada ya Maafa Na. 9 ya mwaka 1990. Sheria hii pamoja na mambo mengine ilianzisha Kamati ya Misaada ya Taifa iliyokuwa na mamlaka ya kupokea na kuidhinisha misaada nchini. Vilevile, Sheria hiyo ilianzisha Idara ya Uratibu wa Misaada ya Maafa katika Ofisi ya Waziri Mkuu. Hata hivyo, Serikali iliendelea kufanya maboresho katika mfumo wa uratibu wa maafa ambapo mwaka 2003 iliandaa Mwongozo wa Taifa wa Operesheni za Menejimenti ya Mafaa ambao uliweka taratibu za operesheni za maafa na kuainisha majukumu ya wadau wa kukabiliana na maafa.
Aidha, mwaka 2004 Serikali ilitunga Sera ya Taifa ya Menejimeti ya Maafa ambayo inatoa mwongozo katika shughuli za usimamizi wa maafa kwa kuzingatia maeneo yote muhimu ya mzingo wa menejimenti ya maafa ambayo ni kuzuia na kupunguza athari za majanga, kujiandaa, kukabiliana na kurejesha hali pamoja na kuimarisha mifumo ya kiutendaji. Vilevile, Sera hii imezingatia masuala ya upatikanaji wa fedha katika kugharamia shughuli za maafa, mifumo ya tahadhari ya mapema, uhifadhi wa mazingira, makundi maalumu, na ushirikiano wa kikanda na kimataifa. Miongozo mbalimbali iliandaliwa kuwezesha utekelezaji wa sera hii ikiwemo mwaka 2015 kutunga Sheria ya Usimamizi wa Maafa, Sura ya 242 ambayo iliifuta Sheria ya Uratibu wa Utoaji wa Misaada ya Maafa Na. 9 ya mwaka 1990. Aidha, Serikali iliendlea kuboresha mifumo ya usimamizi wa maafa ambapo mwaka 2022 ilitunga Sheria ya Usimamizi wa Maafa, Sura ya 242 ambayo ilifuta Sheria ya mwaka 2015 na mwaka 2025 Serikali ilifanya mapitio ya Sera ya mwaka 2004 na kuja na Sera ya Usimamizi wa Maafa ya Mwaka 2004 (Toleo la 2025).
Makujumu
Wizara kupitia Idara, itafanya yafuatayo:
Muundo wa Shirika
Muundo wa Idara ya Usimamizi wa Maafa chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu